Usisimame Sasa
We're glad you like it!
Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.
Mwanzo 6:13,14,22 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia. Ujifanyie safina ya mti wa mvinje; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami … Ndivyo alivyofanya Nuhu, sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.
Dhana ya kifalsafa iitwayo Nihilism (yaani kukana kila kitu) ni imani kwamba maisha, kimsingi, hayana maana yoyote, wala thamani, wala lengo; kwamba kusimamia ukweli wa maadili hakuhitajiki tena, kwa kuwa kunachukuliwa kuwa kumepitwa na wakati. Kwa mtazamo huo, mtu hufikia hitimisho kwamba ni heri tule, tunywe na kufurahi, kwa maana kesho tutakufa. Kwa kuwa watu wengi wanaamini dhana hiyo siku hizi, tunaweza kuuliza swali hili la msingi: Je, unaona imani hiyo inasaidia kweli?
Bila shaka, umewahi kusikia habari za Nuhu—yule jamaa aliyeonekana kana kwamba amechanganikiwa akili, mtu aliyeanza kujenga meli kubwa mno, mbali kabisa na bahari. Yaani, ilikuwa safina kubwa sana, inayofanana kwa ukubwa na meli za kisasa zinazotembea katika bahari kuu. Kwa nini afanye hivyo? Jibu lake lilikuwa rahisi: “Kwa sababu Mungu ndiye aliyeniagiza.”
Nuhu aliishi katikati ya watu waliokana kila kitu na kuishi bila maadili yoyote. Jamii ilikuwa imeharibika kabisa; vurugu, dhuluma, uonevu na udhalimu vilienea kila mahali. Kwa mtazamo wao, hilo lilionekana la kawaida—kwa maana, kama hakuna maana wala lengo la maisha, kwa nini mtu ajizuie?
📖 Mwanzo 6:13,14,22
Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia. Ujifanyie safina ya mti wa mvinje; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami … Ndivyo alivyofanya Nuhu, sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.
Ilichukua miaka mingi kwa Nuhu kufanya “yote aliyomwamuru Mungu”—kujenga ile safina kubwa katikati ya mazingira ya uovu na dhihaka. Ebu fikiria upinzani aliokumbana nao! Ni dhahiri hakukosa kejeli, mashaka na chuki kutoka kwa watu waliomzunguka.
Lakini Nuhu hakusimama kujitetea wala kujieleza kwa kila mtu aliyempinga. Aliendelea tu kufanya kazi aliyokabidhiwa—akaendelea kujenga safina—na akaacha mvua ithibitishe ukweli baadaye.
Angalia, watu watakupinga unapochagua kutenda mema, kumheshimu Mungu au kumfuata Yesu; hilo haliepukiki. Kwao, unaweza kuonekana kama mtu aliyepoteza akili, kama alivyodhaniwa Nuhu. Lakini hata hivyo, endelea kutenda mema. Mheshimu Mungu. Usiache kumfuata Yesu, hata kama inachukua muda mrefu. Matokeo, mwachie yeye.
Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.
