Una Thamani Kiasi cha Mtu Kukubali Kukufia
We're glad you like it!
Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.
Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Tukiingia tena wiki ya kukumbuka Pasaka, ninajiuliza jinsi unavyolithamini swala zima la Pasaka. Tukiliacha lipite tu, labda kwa kufurahia chakula na wikendi ndefu, tunaweza kukosa kuuelewa moyo wa Mungu kwetu. Kwa sababu Pasaka ni namna Mungu anavyokuambia jambo hili: unayo thamani kiasi cha mtu kukubali kukufia.
Kwa hiyo, tuanze kipindi hiki cha Pasaka kwa kuchunguza kwa ujumla maana yake. Katika Zaburi 139, mwandishi ananukuu dua lake kwa Mungu akitukumbusha thamani yetu, kuanzia wakati tulipokuwa bado tumboni mwa mama zetu:
Zaburi 139:13,14 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, uliniunga tumboni mwa mama yangu. Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.
Hii ina maana kwamba Mungu alikuumba kwa vidole vyake mwenyewe. Alikuunga tumboni mwa mama yako. Hukuwepo kwa bahati nasibu tu. Uliumbwa kwa upendo, kwa ajili ya upendo, ili umjue Mungu na kutembea naye. Lakini kulitokea msiba mkubwa:
Warumi 3:23 Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
Kila mmoja wetu, kwa njia yake mwenyewe, amemkosa Mungu. Tumekosa lengo. Na uasi huo sasa unatugharimu.
Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti.
Lakini hata hivyo, Mungu akijua yote haya, bado aliamua kuingilia kati.
2 Wakorintho 5:21 Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.
Aliweka dhambi zetu — za kwako na za kwangu — juu ya Yesu. Kwa nini? Ili tuweze kupata mambo ambayo hatukuyastahili: msamaha, uhuru, na uzima wa milele.
Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Pasaka si jambo la kupita kwa haraka-haraka. Si kukumbuka tu dhabihu aliyotoa Mungu, bali linahusu mwitikio wako kwake yule aliyetoa uhai wake kwa ajili yako. Yule aliyeona mapungufu yako yote, lakini hata hivyo akasema, “Unayo thamani kiasi cha mtu kukubali kukufia.”
Kwa hiyo ninakusihi, usikipitie kipindi hiki cha Pasaka bila kutafakari. Tulia kwanza, fikiria jinsi Yesu alivyokupenda — kwa sababu hakufa kwa ajili ya ulimwengu tu, bali alikufa kwa ajili yako binafsi.
Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.
