Mwelekeo Mmoja
We're glad you like it!
Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.
2 Wakorintho 6:14,15 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
Ni ajabu sana jinsi watu walivyo na mitazamo tofauti-tofauti—katika siasa, mahusiano, na hata kazini, sivyo? Kwa upande mmoja, hili linaweza kuwa jambo jema. Mitazamo mbalimbali inaweza kuchangia mawazo mapya na kuleta matokeo bora zaidi. Lakini kwa upande mwingine, tofauti hizo zinaweza pia kuleta migawanyiko na mtengano.
Basi jiulize swali hili: Unachaguaje watu wanaokuzunguka na kuwa karibu nawe?
Kwa upande mmoja, si busara kutafuta kundi la “watu-ndiyo”—yaani watu wanaokubaliana nawe kila wakati bila kupinga chochote. Hilo ni hatari. Mke wangu amenisaidia sana katika jambo hili; hunikosoa kwa upendo anapoona nimekosea, nami pia humsaidia vivyo hivyo. Hiyo ni afya ya mahusiano.
Lakini kwa upande mwingine, kama watu waliokuzunguka wanapingana nawe kila mara bila kujenga, je, kweli ungependa kuishi katika migongano ya kudumu? Sidhani. Fikiria ingekuwaje kuwa katika ndoa au kazini kwenye mazingira ya namna hiyo—isingekuwa rahisi wala ya kufurahisha hata kidogo.
📖 2 Wakorintho 6:14,15
Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
Ebu fikiria ng’ombe wawili waliofungwa nira isiyo sawasawa—kila mmoja akivuta kwa kasi na mwelekeo tofauti. Watatumia nguvu nyingi sana, lakini hawatasonga mbele.
Sijui wewe ukoje, lakini kile kinachonisukuma mimi—kile kilicho katika kiini cha moyo wangu—ni imani yangu ndani ya Yesu: upendo wake, uwezo wake, neema yake na msamaha wake; pamoja na shauku ya kutenda yaliyo mema na haki machoni pake.
Kujikumbusha: Epukana na kujiunga kwa ukaribu na mtu anayetembea katika mwelekeo tofauti kiroho.Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa.
Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.
