... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Wakati Unatetemeka

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Zaburi 18:2 BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.

Listen to the radio broadcast of

Wakati Unatetemeka


Download audio file

Hofu ni hali ambayo iko sehemu zote, yaani wengi tu wanaogopa kuliko jinsi tunavyofikiria.  Kwa hiyo, sio wewe tu unaogopa.  Hofu inaweza kumshika mtu muda wo wote, hususani akijikuta amekabiliana na shida ambayo hakutegemea.

Wakati nilikuwa jeshini, tukifundishwa mbinu za vita, tuliambiwa kwamba kushutukiza adui ina saidia sana katika mapambano.

Ndiyo maana wanajeshi wanaweka mitego na kuandaa mashambulizi ya ghafla.  Ndiyo maana daima unajaribu kudanganya adui, ili ukimshambulia, asiweze kujua mnatokea wapi wala kujua nguvu za kikosi chako zikoje.

Ebu sikiliza mwitikio wa Daudi, hata kama ilitokea zamani, baada ya Mungu kumwokoa na mkono wa Mfalme Sauli na wengine wote waliojaribu kuangamiza uhai wake:

Zaburi 18:2  BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.

Wengi wetu, wakati masase yanaanza kurushwa, tunakimbia moja kwa moja kuelekea sehemu bunduki zinalia.  Yaani, ni kama tunalenga matatizo yetu badala ya kumgeukia Mungu.

Hii haieleweki, kwa sababu Mungu ndiye Mwamba, boma lako na kimbilio lako.  Kama vile Charles Spurgeon alieleza vizuri, wakati mtu anatetemeka, Mwamba wake anaposimama juu yake hautikiswi!  Mkimbilie yeye ili upate hifadhi.

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.