Kubanwa Mno
We're glad you like it!
Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.
2 Timotheo 3:12,13 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
Siku hizi wengi wanaomwamini Yesu wanabanwa sana. Ni kama wanapinga Injili wamezidi kujikusanya kijeshi dhidi yao.
Sijui kama umeshaiona hiyo? tunashuhudia serikali mbalimbali zinapitisha sheria za kubana uhuru wa ibada, wapinzani wenye itikadi kali pamoja na nguvu za uovu wanazidi kupiga kelele kwa kujaribu kunyamazisha sauti za wakristo ili ionekane kama wametushinda.
Ndipo tunasikia sauti inaibuka ndani yetu na kusema: Haitakiwi iwe hivyo! Kama Mungu ni Mfalme wa wafalme, kwanini haingilii kati? Kwanini najisikia kuudhiwa kwasababu ya imani yangu?
Hayo yote si mapya kwenu. Inategemeana. Huko kwetu, mimi nimekuwa nikiona wanatetea sana ukristo, sasa kule kuudhiwa kunatupiga kama mawimbi makali … ndio maana nasema,“tumeanza kubanwa mno.”
Lakini tusingeshangaa hata kidogo, Kama vile Paulo alivyomwandikia Timotheo miaka 2000 iliyopita:
2 Timotheo 3:12,13 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
Umempata vizuri? Imeandikwa “wote” bila kuacha hata mmoja. Kama kweli umeambatana na Kristo, utaudhiwa. Pia imeandikwa kwamba hali hiyo itaendelea na kuzidi. Ndivyo ilivyo leo, si kweli?
Lakini bado kuna habari njema. Wale waovu, wanadanganyika tu. Kumbuka kwamba Mfalme wako bado anatamalaki kwenye kiti chake cha enzi.
Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.